HIVI SASA NI SAA

TAREHE

Thursday, November 5, 2009

UFAHAMU MLIMA WA OL DOINYO LENGAI


Ol Doinyo Lengai (Kimaasai "mlima wa Mungu") ni mlima wa volkeno katika Tanzania ya Kaskazini. Iko takriban 120 km kaskazini-magharibi ya Arusha. Iko 25 km kusini ya Ziwa la Magadi (Tanzania - "Lake Natron").
Jina la mlima ni Kimaasai lamaanisha "mlima wa Mungu". Mlima una kimo cha 2690 m juu ya UB. Ni volkeno ya pekee duniani kutokana na aina ya lava yake inayotoka hali ya kiowevu (majimaji) lakini si moto sana (mnamo 500° - 600 °C).
Ol Doinyo Lengai ilipuka tena katika Machi 2006. Katika mwaka 2007 mlima umesababisha mitetemeko ya ardhi ya mara kwa mara kuanzia 12 Julai. Tetemeko la 18 Julai lilisikika hadi Nairobi.

No comments: